Friday, 23 March 2018

WANANCHI HAI WATAKIWA KUCHUKUA TAHADHARI YA KUJIKINGA NA UGONJWA WA KICHAA CHA MMBWA






 Na Salma Shabani

 HAI


Wananchi wilayani Hai mkoani Kilimanjaro wametakiwa kuchukua taadhari ya kujikinga na ugonjwa wa kichaa cha Mbwa ulioripotiwa kuua watu watatu wilaya ya moshi vijijini.


Akizungumza na redio boma hai fm Mganga mkuu wa Hospitali ya wilaya ya hai Daktari Irine Haule amesema kuwa kila mwananchi anapaswa kuchukua taadhari hiyo pamoja na watoto wadogo kuwa karibu na familia zao kwa ulinzi zaidi.


Ameongeza kuwa kila mwananchi anapaswa kuchukua taadhari za kufika katika vituo vya afya pindi wanapo ng’atwa na mbwa wanao zurura hovyo na kuwataka waripoti katika vituo vya afya ili waweze kupatiwa tiba.


Haule amewataka wamiliki wa mbwa kuwachanja  mbwa wao wanao wafuga ili kuondokana na ugonjwa huo ikiwa ni pamoja na wamiliki wa mbwa hao kuwafungia ndani kipindi cha mchana kwa taadhari zaidi  kwani mbwa kuzurura hovyo ni kuhatarisha maisha ya watu jambo ambalo ni kosa kisheria.


Ugonjwa wa kichaa cha mbwa ni moja ya magonjwa yanayo athiri maeneo mengi duniani,maradhi yanayo sababishwa na virusi kutoka kwa wanyama jamii ya mbwa walio athirika na virusi hivyo,wakiwemo,fisi,paka na mbweha.


Inakadiriwa kuwa kati ya asilimia  30-50 ya waathirika wa ugonjwa wa kichaa cha mbwa ni watoto wenye umri chini ya miaka 15.

No comments:

Watumiaji wa Barabara Watakiwa Kutii Sheria za Usalama

Mkuu wa Kitengo cha Usalama barabarani Mkoa wa Kilimanjaro Mrakibu Msaidizi wa Polisi Sauda Mohamed akizungumza na wananchi kwenye ...