Meneja wa TARURA Wilaya ya Hai Mhandisi Charles Marwa (kulia) akitoa maelezo katika kijiji cha sanya station katika kata ya Kia baada yakukumbwa na mafuriko. |
![]() |
Mkuu wa wilaya ya Hai Mh. Onesmo Buswelu Akitoa maelekezo kwa viongozi wa kijiji cha sanya station, pamoja na maafisa mazingira wilaya mara baada ya kijiji hicho kukumbwa na mafuriko. |
![]() | |
Mkazi wa kijiji cha sanya station akizungumzia athari ziliz |
![]() |
Eneo ambalo mto umeacha njia yake rasmi nakutengeneza mto mwingine pembeni mara baada ya mvua kubwa kunyesha katika kijiji cha sanya station kata ya Kia wilayani Hai( Picha zote na Davis Minjer) |
NA Adrian Lyapembile na Davis Minja
HAI
Mkuu wa Wilaya ya Hai mkoani Kilimanjaro Mhe. Onesmo Buswelu
amewaagiza wataalamu wa mazingira, kilimo na Wakala wa Barabara Vijijini na
Mijini (TARURA) kushirikiana kufanya usafi ndani ya mto Sanya eneo la Sanya
Staion kuondoa mlundikano wa mchanga kwenye kina cha mto huo pamoja na kupanda
miti na makingamaji kwenye eneo la mto alipofanya ziara ya kukagua madhara
yaliyosababishwa mvua zinazoendelea kunyesha na kufanya mto kuacha njia ya
asili na kuanzisha mkondo mwingine.
Buswelu ametoa agizo hilo hapo jana alipofika eneo la ardhi
lililoharibiwa na maji ambayo yameanzisha mto mwingine unaoelekea kwenye
mashamba na makazi ya wananchi wa kijiji cha Sanya Station katika kata ya Kia
na kusababisha uharibufu wa mazao.
Mkuu huyo wa Wilaya pia ameliagiza jeshi la Mgambo wilaya ya
Hai kushirikiana na wananchi katika kutoa nguvu kazi wakati wa zoezi la
kusafisha mto huo kwa lengo la kukamilisha kazi hiyo kwa haraka ili kuzuia
uharibifu mwingine unaoweza kutokea kutokana na mvua zinazoendelea kunyesha.
Pamoja na agizo hilo, Buswelu amewataka wananchi wanaoishi
maeneo ya jirani na mto huo kuchukua hatua za kutunza mazingira kwa kuotesha
miti na kuacha kufanya shughuli za kibinadamu ikiwemo kilimo ndani ya mita 60
kutoka eneo la mto.
Akizungumzia uharibifu uliojitokeza kwenye mazao ya wakulima,
kaimu mtendaji wa kata ya Kia Simba Lema amesema zaidi ya ekari 477 zimepitiwa
na maji na kwamba tathmini inaendelea kufanywa ili kubaini gharama halisi ya madhara
yaliyopatikana kwenye mazao.
Naye meneja wa TARURA wilaya ya Hai mhandisi Charles Marwa
amesema kutokana na umuhimu wa mto huo kwa jamii watasimamia zoezi hilo kwa
kutoa ushauri wa kitaalam na kwa haraka zaidi kama walivyoagizwa na Mkuu wa
wilaya ili kuwawezesha wananchi
walioathiriwa na kuchepuka kwa mto huo kuendelea na shughuli za kijamii na
kiuchumi.
No comments:
Post a Comment