Friday, 23 March 2018

Kichaa cha mmbwa tishio kilimanjaro





MOSHI

Idara ya Mifugo na Uvuvi katika halmashauri ya Wilaya ya Moshi mkoani Kilimanjaro,  imefanikiwa kuwaua mbwa wenye kichaa 96 kutoka katika kijiji cha Mawala, Mikocheni, Msekia na Mtakuja.


Akizungumza katika mahojiano maalum na mwandishi wa habari ofisini kwake afisa Mifugo na uvuvi Dkt Walter Marandu, alisema kuwa halmashauri imechukua hatua za haraka za kuwaua mbwa hao lengo likiwa ni kuwadhibiti wasiendelee kuleta madhara kwa binadamu.

Alisema kuwa tatizo la uwepo wa ugonjwa wa kichaa cha mbwa ni mkubwa, wapo mbwa wengi wenye ugonjwa huo na takwimu tulizonazo kuanzia kipindi cha Januari hadi Machi mwaka huu watu waliong’atwa na mbwa wafikia 64.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa halmashauri ya Moshi, Marco Kilawila alisema kuwa tayari halmashauri hiyo imeshaanza zoezi la kuwachanja mbwa wote.

Hata hivyo aliwataka wamiliki wote wa mbwa kuhakikisha kuwa  wanapatiwa chanjo zinazositahili kuanzia chanjo ya kichaa cha mbwa, pamoja na magonjwa mengine ili kuepusha watu wasiendelee kupata madhara zaidi.

No comments:

Watumiaji wa Barabara Watakiwa Kutii Sheria za Usalama

Mkuu wa Kitengo cha Usalama barabarani Mkoa wa Kilimanjaro Mrakibu Msaidizi wa Polisi Sauda Mohamed akizungumza na wananchi kwenye ...