Wednesday, 24 January 2018

RAIS MAGUFULI ATUMA SALAMU






Rais Dkt. John Magufuli ametuma salamu za rambirambi kwa Jaji Mkuu wa Tanzania, Prof. Ibrahimu Juma kufuatia kifo cha Jaji Mstaafu wa Mahakama ya Rufani, Mh. Robert Kisanga kilichotokea tarehe 23, Januari mwaka huu. 


Katika salamu hizo Dkt. Magufuli amesema Jaji Mstaafu Robert Kisanga atakumbukwa kwa mchango wake mkubwa alioutoa kwa taifa wakati wote wa utumishi wake uliojaa umakini, uchapakazi, uzalendo na ushirikiano na wengine.


Mh Raisi amewaombea wafiwa wote wawe na moyo wa subira,uvumilivu na ustahimilivu katika kipindi hiki kigumu cha majonzi na amemuombea marehemu Jaji mstaafu Kisanga apumzishwe mahali pema peponi, amina.



Watumiaji wa Barabara Watakiwa Kutii Sheria za Usalama

Mkuu wa Kitengo cha Usalama barabarani Mkoa wa Kilimanjaro Mrakibu Msaidizi wa Polisi Sauda Mohamed akizungumza na wananchi kwenye ...