Tuesday, 12 December 2017

WENYEVITI WA VITONGOJI WATAKIWA KUSIMAMIA ULINZI NA USALAMA




Inspector Shabo wa kituo cha polisi Bomang'ombe wakati akizungumza katika kikao cha mamlaka ya mji mdogo wa Hai

Mwenyekiti wa mtaa wa Kingereka B, Saidi Seifu Mkambala wakati akizungumza katika kikao cha kamati ya mamlaka ya Mji mdogo wa Hai

Na Praygod Munisi

HAI
Viongozi wa serikali za mitaa wilayani Hai mkoani Kilimanjaro wametakiwa kusimamia ulinzi na usalama katika mitaa yao na kuhakikisha linaimarika hasa katika kipindi hiki cha mwishoni mwa mwaka.

Hayo yamesemwa  na inspekta Shabo wa kituo cha polisi Bomang’ombe wakati wakufanyika kwakikao cha kamati ya mamlaka ya mji mdogo wa Hai,nakusisitiza kuwa viongozi hao wakiwa kama walinzi wa Amani katika mitaa, hivyo ni vyema kuhakikisha usalma na mali za Wananchi zinakuwa salama muda wote nakuhakikisha wanatokomeza kabisa vitendo vya ualifu katika mitaa yao kwakushirikiana na jeshi la polisi.

Shabo amesisitiza kuwa viongozi wa serikali za mitaa ni vyema wakatumia vikundi vya ulinzi shirikishi vilivyopo katika mitaa yao ili vishirikiane na jeshi la polisi katika kupambana na kupunguza uhalifu kwenye mitaa nakuwakumbusha wananchi umuhimu wakutumia hivi vikundi.

‘’tuwakumbushe watu wetu hivi vikundi ambavyo tulivyonavyo vifanye kazi ili tuweze kupunguza ualifu ambao unaendelea kutokea’’alisema shabo.

Kwa upande wake mwenyekiti wa mtaa wa kingereka B katika mji wa Bomang’ombe Bw.Saidi Seifu Mkambala amelishauri jeshi la polisi wilayani Hai kuzidi kuimarisha doria katika mitaa hususa nikatika mji wa bomang’ombe kutokana nakuongezeka kwa vitendo vya kiualifu nakuwaomba viongozi wenzake wa serikali za mitaa kutoa ushirikiano wakutosha kwa jeshi hilo ili suala la ulinzi na usalama lizidi kuimarika.

No comments:

Watumiaji wa Barabara Watakiwa Kutii Sheria za Usalama

Mkuu wa Kitengo cha Usalama barabarani Mkoa wa Kilimanjaro Mrakibu Msaidizi wa Polisi Sauda Mohamed akizungumza na wananchi kwenye ...