Thursday, 1 March 2018

Vurugu za wanafunzi zasababisha shule kufungwa kwa muda Hai

NA OMARY MLEKWA

HAI
 
SERIKALI wilaya Hai mkoani Kilimanjaro imeifunga shule ya Sekondari ya Lyamungo kwa zaidi ya wiki mbili baada ya Wanafunzi kufanya vurugu na uharibifu wakipinga mwenzao kufukuzwa shuleni hapo.


Hatua hiyo inatokana na uharibifu mkubwa uliofanywa na wanafunzi hao kwa kuharibu miundombinu ya shule hiyo ikiwemo nyumba  ya mwalimu wa  nidhamu wa  shule hiyo.

Mkuu wa  wilaya hiyo mshikizi Onesmo Buswelu alisema hatua ya kuifunga shule hiyo ni ili kuepusha uharibu zaidi pamoja na uvunjifu wa  amani.

"Kamati ya ulinzi na usalama imeridhia wanafunzi wote kuondoka shuleni na kwenda kwa wazazi  wao na wanapaswa kurejea shuleni Machi  18 mwaka huu"aliseama

" Wanafunzi walifanya vurugu na fujo  na hatimaye  maandamo siku ya Feb 28 kwa lengo la  kumwona mkurugenzi wa  Halmashauri ya wilaya kuyokana na mwanafunzi mwenzao kuadhibiwa na mwalimu wa  Nidhamu wa shule hiyo Safari Lasini "alisema

" Maandamo hayo yalikwamia katika eneo la  Mashine Tools ambapo walikutana na Kaimu mkutugenzi wa  Halmashauri ,Edward Ntakilio na wanafunzi  walitii na kurejea shuleni "alisema 

" Mwanafunzi wa  kidato cha tano  ,Moses Siima anayesoma mchepuo wa  HGE,anadaiwa kuwatukana waalimu jambo ambalo lilisababisha  kuadhibiwa pamoja na kusimamishwa masomo"alisema

Akitoa maamuzi hayo kwa wanafunzi hao Machi  moja mwaka huu,kaimu mkurugenzi Ntakilio alisema wanafunzi  watarejea shuleni hapo Machi 18 mwaka huu na endapo mwanafunzi atakosa kuripoti atahesabiwa kuwa mtoro.

"Maamuzi haya ni ya awali itaundwa kamati kwa ajili ya ufuatiliaji na kufanya tathimini ya uharibifu huo ili hatua zaidi za kisheria" alisema

No comments:

Watumiaji wa Barabara Watakiwa Kutii Sheria za Usalama

Mkuu wa Kitengo cha Usalama barabarani Mkoa wa Kilimanjaro Mrakibu Msaidizi wa Polisi Sauda Mohamed akizungumza na wananchi kwenye ...