Friday, 9 March 2018

UKOSEFU WA SOKO LA UHAKIKA WA BIDHAA ZA NGOZI WAPELEKEA WAFANYA BIASHARA KUOMBA KUUZA BIDHAA HIYO NJE YA NCHI





Na Salma Shabani

SIHA,

Wafanayabiasha wa bidhaa za Ngozi Wilayani Siha Mkoani Kilimanjaro,wameomba Serikali kuwaruhusu kuuza bidha hiyo nje ya nchi kutokana na kukosa soko la uhakika hapa nchini


Wakizungumza na waandishi wa habari  kwa nyakati tofauti wafanyabiashara hao waamesema kuwa tangu kuwekwa kwa masharti ya kusafirisha bidhaa hiyo nje ya nchini wamekuwa wakipata hasara kutokana na kukosa soko la uhakika hapa nchini

Mmoja wa wafanyabiashara hao ,Zakaria Materu amesema kuwa tangu mwaka 2015 kumekuwepo mlundikano wa ngozi nyingi hali ambayo imesababisha kuendelea kuishi maisha magumu

Amesema serikali wakati ikiwakwenye mchakato wa ufufuaji wa vyema vya ngozi hapa nchini ni vyema wakawaruhusu kuendelea na kuuza ngozi nchi ya nchi ili kunusuru wafanyabiashara hao kupata hasara

Alisema kabla ya zuio la Serikali wafanyabiashara kutoka Nchini Kenye walikuwa wakinunua  kwa shilingi 8000 hadi 5000 ngozi moja lakini kwa sasa hakuna anayeuliza bei

Nae mfanyabiashara e Lasteck Gideon,alisema wakati serikali ikijipanga kuingia kwenye uchumi wa viwanda ingewaruhusu kuuza ngozi hizo ili kulinda mitaji yao,sambamba na kuiongezea serikali mapato

Afisa mifugo wa Wilaya hiyo Barnabas Mbwambo,alisema kuwa Ngozi zipo nyingi sana kwenye wilaya yake, sina idadi ya tani lakini ni nyingi hata Wilaya za jirani tunamawasiliano nao wanadaia ngozi ni nyingi na kwamba hakuna soko

No comments:

Watumiaji wa Barabara Watakiwa Kutii Sheria za Usalama

Mkuu wa Kitengo cha Usalama barabarani Mkoa wa Kilimanjaro Mrakibu Msaidizi wa Polisi Sauda Mohamed akizungumza na wananchi kwenye ...