Friday, 9 March 2018

WANAWAKE WASHAURIWA KUJIUNGA NA VIKUNDI VYA UJASIRIAMALI ILI KUFIKIA UCHUMI WA VIWANDA




 Na Edwine Lamtey

HAI.

Wanawake wametakiwa kujituma na kujiamini katika shughuli mbali mbali za kiuchumia hapa nchini ikiwa ni pamoja na uzalishaji mali kwa njia ya kujiunga katika vikundi vya ujasiriamali ili kuweza kujikimu katika maisha ya sasa  pamoja na kufikia uchumi wa viwanda .


Hayo yamesemwa mapema hii leo na katibu tawala wilaya ya Hai Bi Upendo Wella wakati wa maadhimisho ya siku ya wanawake duniani yaliyofanyika kata ya masama rundugai wilayani hai mkoani Kilimanjaro na kushirikisha wanawake mbali mbali kutoka maeneo ya wilaya ya Hai.

Upendo Amesema ni vyema wanawake wakajiunga katika vikundi mbali mbali vya ujasiriamalikwa lengo la  kuanzisha viwanda vidodogo vidogo kwa kutumia fursa za mikopo ya wanawake na vijana zinazotolewa  na Halmashauri

Kwa upande wa wadau mbali mbali waliohudhuria maadhimisho hayo, mwenyekiti wa dawati la Jinsia na watoto wilayani Hai Coplo Happness Eliufoo amesema kuwa kwa sasa wanawake wanapaswa kuzidi kusimama na kuendana na kasi ya kuelekea uchumi wa viwanda badala ya kusubiri kuinuliwa kama ilivyokuwa hapo awali.

Naye  mwakilishi wa shirika lisilo la kiserikali la voice of empowered women foundation bi lightness kimaro amesema kutokana na kuthamini mchango mkubwa unaotolewa na wanawake katika jamii shirika lao limeweza kuwasaidia wanawake mbalimbali ambao wanakutana na changamoto ambazo zinawakabili pamoja na kupinga vitendo vya ukatili wanavyofanyiwa wanawake.

Kwa upande wake mkuu wa idara ya maendeleo ya jamii Bwana lukasi msele amesema kuwa idara yamaendeleo ya jamii wilaya ya Hai bado inazidi kuhamasisha na kutoa elimu juu ya kujiunga na vikundi mbali mbali pamoja na kuwaelekeza njia sahihi ya kutumia fursa hizo za mikopo ambapo wilaya ya Hai imekwishatoa mikopo hiyo kwa zaidi ya vikundi vitano vya wanawake.

Kauli mbiu ya siku ya wanawake mwaka huu ni :kuelekea uchumi wa viwanda tuimarishe uchumi wa jinsia na uwezeshaji wanawake vijijini.

No comments:

Watumiaji wa Barabara Watakiwa Kutii Sheria za Usalama

Mkuu wa Kitengo cha Usalama barabarani Mkoa wa Kilimanjaro Mrakibu Msaidizi wa Polisi Sauda Mohamed akizungumza na wananchi kwenye ...