Wednesday, 7 March 2018

SERIKALI KILIMANJARO YASHAURIWA KUTOA ELIMU KWA WAVUVI



 

Mwenyekiti wa Chama cha ACT wazalendo Mkoa Wa Kilimanjaro mwalimu Mgala Ramadhani [katikati} wakati akizungumza na waandishi wa Habari Kilimanjaro.[picha na Edwine Lamtey]



Na Edwine Lamtey

MOSHI

Serikali imeshauriwa kutafuta njia mbadala ikiwemo ya utoaji wa elimu na ukamataji wa wavuvi haramu katika kulinda rasilimali zilizopo ndani ya bwawa la Nyumba ya Mungu badala ya kulifunga ambapo hali hiyo imedaiwa kuathiri wananchi wanaotegemea shughuli za uvuvi katika bwawa hilo.

Akitoa rai hiyo mwenyekiti wa chama cha ACT wazalendo mkoa wa Kilimanjaro mwalimu Mgala Ramadhani amesema kuwa badala ya serikali kuwekeza nguvu kubwa katika kukamata na kufanya msako wa samaki katika soko la Manyema ni vyema serikali ikaweka mkakati wa kuwachukulia hatua wanaotumia zana zisizo stahili katika bwawa hilo pamoja na kutoa elimu kwa wananchi juu ya njia sahihi ya kufanya uvuvi.

Kauli hiyo ya ACT inakuja baada ya agizo la mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Bi Anna mghwira kulifunga bwawa la Nyumba ya mungu kwa kile kilichoelezwa kuwa samaki wanaovuliwa ni wadogo kupita kiasi na hivyo kuamua kulifunga bwawa hilo.

Kwa upande wake katibu wa chama hicho Ally Mdimu amesema kuwa badala ya nguvu kubwa kutumika kuwasaka wanaoingiza samaki katika soko la manyema ni vyema nguvu hiyo ikaelekezwa katika kulinda bwawa hilo kwani hata samaki hao wanapokamatwa katika soko hilo ni dhahiri kuwa uharibifu umekwishafanyika na haiwezekani kuwarudisha tena katika bwawa hilo.

Sanjari na hayo katibu huyo amepongeza juhudi zinazofanya na serikali na kusema kuwa chama cha ACT wazalendo kitazidi kuunga mkono jitihada nzuri katika kuheshimu misingi ya utawala bora huku kikipinga siasa za majungu na wasiopenda maendeleo.

No comments:

Watumiaji wa Barabara Watakiwa Kutii Sheria za Usalama

Mkuu wa Kitengo cha Usalama barabarani Mkoa wa Kilimanjaro Mrakibu Msaidizi wa Polisi Sauda Mohamed akizungumza na wananchi kwenye ...