Wednesday, 7 March 2018

CCM HAI YACHANGIA VIFAA VYA UJENZI KWAAJILI YA UKARABATI WA SHULE




HAI 
CHAMA cha mapinduzi (CCM) Wilayani Hai Mkoani Kilimanjaro kimetoa msaada wa vifaa vya ujenzi katika shule ya msingi Kibohehe kwa lengo la kukarabati shule hiyo ambayo iliezuliwa paa na kuharibika miundombinu yake na kusababisha kifo cha mwanafunzi mmoja wa darasa la Sita 


Hatua ya CCM  ya kuwapatia vifaa hivyo vya ujenzi ili kuharakisha ukarabati wa vyumba vya madarasa ili wanafunzi waweze kurejea shuleni hapo ambapo kwa sasa wamehamishiwa katika shule za jirani 

Akizungumza na wajumbe wa serikali ya kijiji pamoja na wataalamu wakati akikabidhi msaaada huo Mwenyekiti wa CCM, Wilaya ya Hai, Wang’uba Magai amesema chama cha mapinduzi kitakuwa bega kwa bega  kuhakikisha wanatoa msaada pale utakapohitajika ikiwa ni pamoja na kufuatilia  shughuli nzima ya ujenzi shuleni hapo.

Msaada uliotolewa shuleni hapo ni pamoja na mifuko 37 ya  sementi, misumari kilo 10 pamoja na chokaa ambapo ujenzi huo  utaanza na vyumba sita vya madarasa .

Kwa upande wake mkuu wa Wilaya ya Hai mshikizi  mhe, Onesmo Buswelu  ameunga mkono jitihada za mwenyekiti wa CCM kwa kuongeza mifuko 10 ya sementi na matofali elfu moja kwa lengo la kusaidia ujenzi  huo kwenda haraka ili wanafunzi waweze kurejea shuleni hapo.

Nae  mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Hai, Yohana Sintoo  amesema kwenye fedha za miradi ya maendeleo  wameweka kiasi cha shilingi milioni moja na hamsini  ambapo fedha hizo zikipatikana  zitasaidia ukarabati wa madarasa hayo kukamilika haraka  kabla ya mwezi wa sita na wanafunzi kurejea.

Shule ya msingi Kibohehe ,ilipata maafa baada ya Ukuta wake kuanguka Mnamo Februari 22 mwaka huu na kusababisha kifo cha mwanafunzi mmoja huku wengine watatu wakijeruhiwa na serikali kuamuru kufungwa kwa muda kupisha ukarabati

No comments:

Watumiaji wa Barabara Watakiwa Kutii Sheria za Usalama

Mkuu wa Kitengo cha Usalama barabarani Mkoa wa Kilimanjaro Mrakibu Msaidizi wa Polisi Sauda Mohamed akizungumza na wananchi kwenye ...