Tuesday, 6 March 2018

Madereva bodaboda chanzo cha ujauzito kwa wanafunzi wilayani Hai.

Na Zaina Andrea na Agness  Mchome
HAI
Madereva wa Boda boda wilaya ya Hai mkoani Kilimanjaro  wamebainika kuwa ndilo kundi linalosababisha kuwapa ujauzito  wanafunzi hasa wale wa sekondari wilayani Hai.

Hayo yamebainishwa na afisa wa Jeshi la polisi kitengo cha dawati  jinsia Wilayani Hai koplo John Maziku wakati akizungumza na Redio Boma Hai fm na kusema kuwa kundi la Madereva wa Bodaboda na Bajaji ndio wanaohusika na suala la kuwapa ujauzito wanafunzi  hasa wale wa shule za sekondari.
Kwa upande wao baadhi ya madereva wa Bodaboda wilayani Hai wamesema kuwa baadhi ya wanafunzi wakati mwingine wanashindwa kujitambua kwa kutojua ni nini wajibu wao hasa katika suala la kuzingatia masomo yao.
Wakizungumzia suala hili nao wanafunzi  wameeleza kuwa mambo hayo hufanyika kwani wanafunzi wengine wanaishi mbali na makazi yao hivyo  huamua kuchukua bodaboda na ndipo wanapowarubuni na kujihusisha na suala la kimapenzi na hatimaye kuapata ujauzito

No comments:

Watumiaji wa Barabara Watakiwa Kutii Sheria za Usalama

Mkuu wa Kitengo cha Usalama barabarani Mkoa wa Kilimanjaro Mrakibu Msaidizi wa Polisi Sauda Mohamed akizungumza na wananchi kwenye ...