Tuesday, 13 February 2018

WAZIRI AFAFANUA KUHUSU FEDHA ZINAZOTOLEWA NA SERIKALI WILAYA YA SIHA

Na Omary Mlekwa
Siha

WAZIRI wa Afya ,Maendeleo ya Jamii ,Jinsia Wazee na Watoto Ummy Mwalimu amesema fedha zinazotolewa na serikali katika Halmashauri ya Siha sio rushwa kutokana  na jimbo  hilo kuwa kwenye mchakato wa uchaguzi  bali  ni utekelezaji wa ilani ya CCM ya mwaka 2015.

WAZIRI wa Afya ,Maendeleo ya Jamii ,Jinsia Wazee na Watoto Mh. Ummy Mwalimu,akimnadi mgombea Ubunge Jimbo la Siha Dr Godwin Molel kwa tiketi ya chama cha mapinduzi CCM.(picha na Omary Mlekwa)

 Akihutubia wananchi wa kijiji cha Louwang kata ya  Donyomurwa katika mkutano wa  kumnadi Mgombea ubunge wa jimbo  hilo kwa tiketi CCM, Dkt Godwin Moleli alisema serikali inadhamiria kuboresha huduma mbalimbali  za kijamii

Alisema serikali itaendelea kuleta fedha za utekelezaji wa miradi na kinachohitaji ni wananchi kuendelea kuiamini serikali ya awamu ya tano kwa kumchagua Mgombea wa CCM, Dkt Moleli.

Alisema kuwa ,kabla ya kujiuzulu nafasi ya Ubunge  Dkt Moleli licha ya kuwa alikuwa mbunge wa upinzani alimwomba fedha za ujenzi wa kituo cha Afya ambapo serikali iliahidi kumpatia kiasi cha shilingi milioni 700 kwa ajili ya ujenzi wa kituo cha Afya Naibilie kata ya Makiwaru

Alisema ,serikali ilikuwa  ikiipatia  hospitali ya wilaya ya Siha kiasi cha shilingi i Milioni 17 kwa mwaka kwa ajili ya madawa  lakini kwa sasa inapokea kiasi cha shilingi milioni44  kwa mwaka  

Alisema kuwa serikali imeongeza fedha katika Vituo vya afya 2 na zahanati 9 ambapo ilikuwa  ikipokea   shilingi Milioni 38 mwaka ila kwa sasa fedha hizo zimeongezeka na kufikia kiasi cha shilingi milioni 175 mwaka

No comments:

Watumiaji wa Barabara Watakiwa Kutii Sheria za Usalama

Mkuu wa Kitengo cha Usalama barabarani Mkoa wa Kilimanjaro Mrakibu Msaidizi wa Polisi Sauda Mohamed akizungumza na wananchi kwenye ...