Na Omary Mlekwa
Siha
USHIRIKIANO kati ya idara ya Elimu sekondari na wadau wa elimu umechangia kuongeza hali ya ufauli kwa watahiniwa wa mtihani kidato cha nne katika Halmashauri ya Siha Mkoani Kilimanjaro.
Halmashauri hiyo imeweza kushika nafasi ya pili kimkoa na nafasi ya 16 kitaifa mwaka 2017 ikilinganishwa na nafasi ya 5 kimkoa na ya 40 kitaifa mwaka 2016.
Akitoa taarifa katika baraza la madiwani ,Mwenyekiti wa Halmashauri hiyo,Frank Tarimo alisema jitihada zilizoonyesha na idara ya Elimu Sekondari zinahitajika ili kuendelea kufanya vizuri,
"Idara ya elimu pamoja na walimu wamefanya kazi nzuri sana ambapo wameweza kuboresha sana matokeo ya mwaka huu ambapo halmashauti yetu tumeshika nafasi ya pili kimkoa na ya kumi na sita kitaifa kati ya Halmashauri ya 194" alisema Tarimo
Alisema katika mtihani wa kitaifa wa kidato cha nne mwaka 2017 jumla ya watahiniwa 912 walifauli katika daraja la kwanza hadi la nne kati ya watahiniwa 1137 waliofanya mtihani .
"Wilaya yetu imeweza kuongeza ufaulu kwa kiwango kikubwa kwani katika mwaka 2016 tulifanya vibaya ambapo shule moja iliingia nafasi ya kumi bora kwa kushindwa kufanya vizuri" alisema
Kwa upande wake ,kaimu mkurugenzi wa Halmashauri hiyo,Saro aliwataka kuhakikisha kuwa wanawafuatikia wanafunzi ambao wamekuwa watoro pamoja na kuwashauri wazazi kuwapatia huduma zote zinazostah
Alisema wilaya hiyo,inajumla ya shule kumi na saba ambapo shule 13 zinamilikiwa na serikali huku shule 4 zikimilikiwa na taasisi binafsi .
No comments:
Post a Comment