Afisa Elimu Sekondari Wilaya ya Hai, Julius Kakyama akisisitiza jambo kwenye kikao cha walimu na wazazi wa wanafunzi. (Picha zote na Praygod Munisi) |
HAI
Wakuu washule za secondary za serikali wilayani Hai mkoani Kilimanjaro wametakiwa kuanzisha jukwaa la wazazi na waalimu ndani ya mwezi mmoja ikiwa ni sehemu ya majukumu yao ili kujadiliana mambo mbalimbali kuhusu maendeleo ya shule na wanafunzi.
"yote kwa yote waalimu wakae darasani watoe kazi,yaani mimi nawataka watoto wakose muda,wapate muda wakusoma tu hizi ziro tunaziondoa mabegi yachekiwe kila mwalimu akiingia darasani ajue mtoto gani yupo,kila mwalimu anapaswa kuwa na daftari la atendensi ya darasa lake kwa watoto wake kila akiingia ajue watoto wote wapoo’’ amesema Kakyama.
Kwa upande wao wazazi wamelalamikia kukithiri kwa utoro na uzururaji wawanafunzi nje ya eneo la shule muda wa masomo na kuwepo kwa wanafunzi wanaomiliki simu shuleni hapo kinyume na taratibu, huku wakioji utaratibu uliopo unaowaruhusu wanafunzi kuwa nje ya eneo la shule muda wa masomo jambo lililopelekea kuomba kuwekewa uzio katika shule hiyo, na kuwaomba waalimu kushirikiana nao ilikuakikisha wanafunzi wanakuwepo shuleni hapo muda wote wa masomo,jambo lilopelekea afisa elimu kumwagiza mkuu wa shule hiyo kuchukua hatua mara moja kwa wanafunzi watoro na mwanfunzi atakae kamatwa na simu shuleni hapo .
"watoto wale wa bweni huwa tunawapa simu ili kumonita kwasababu pengine wanaenda mbali na wakifika huwa wana kabidhi,lakini Yule mtoto anaekuja anarudi jioni unampa simu ya nini,yakufanya nini?hizo simu zote zinapokamatwa ni kupasua ndio msimamo wa serikali hatuna msimamo mwingine zaidi ya huo’’amesema Kakyama.
No comments:
Post a Comment