Thursday, 8 February 2018

WAANDISHI WAHABARI WATAKIWA KUTUMIA VYEMA MAFUNZO WANAYOYAPATA.







Mwenyekiti wa Mtandao wa Redio za Jamii Tanzania –TADIO  ndugu PROSPER KWIGIZE akizungumza na washiriki wa mafunzo katika ukumbi wa TBA
  Mkufunzi Mwandamizi wa Radio za kijamii kutoka  Shirika la Umoja Wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni –UNESCO Bi Rose Mwalimu akifundisha.





Waandishi wa Habari kutoka Redio za Kijamii Tanzania wametakiwa kutumia
fursa zinazotolewa na Shirika la Umoja Wa Mataifa la Elimu, Sayansi na
Utamaduni –UNESCO- ili kuleta mabadiliko kwa Jamii.

Hayo yamesemwa na Mwenyekiti wa Mtandao wa Redio za Jamii Tanzania –TADIO  ndugu PROSPER KWIGIZE katika mafunzo yanayoendelea mjini Dodoma na kwamba  mafunzo ya kitaaluma kama hayo utolewa kwa kulipia ila UNESCO utoa mafunzo kama hayo bila malipo yoyote.

Amesema ni vyema kuthamini na kuzingatia elimu wanayoipata waandishi
katika mtandao wa TADIO na kuifanyia kazi kwa manufaa ya jamii.

Naye Mkufunzi Mwandamizi wa Radio za kijamii kutoka  Shirika la Umoja Wa Mataifa la Elimu, Sayansi na Utamaduni –UNESCO Bi Rose Mwalimu amewataka wamiliki wa vyombo vya habari nchini  kutoingilia uhuru wa  wanahabari katika vituo vyao kwa sababu vinaongozwa na sera na misingi ya taaluma ya habari.



Amesema ni vyema wanahabari wakawa huru katika kutimiza wajibu wao
kitaaluma ili kuihudumia jamii na kujiepusha na masuala binafsi.

No comments:

Watumiaji wa Barabara Watakiwa Kutii Sheria za Usalama

Mkuu wa Kitengo cha Usalama barabarani Mkoa wa Kilimanjaro Mrakibu Msaidizi wa Polisi Sauda Mohamed akizungumza na wananchi kwenye ...