Sunday, 4 February 2018

WATAKIWA KUTUMIA VIZURI TEKINOLOJIA YA TEHAMA KWA SHUGHULI ZA MAENDELEO

Na Elisha Eliakimu  HAI

Katibu tawala wilaya ya Hai Bi Upendo Wela amewataka mahakimu kutumia vizuri tekinolojia ya tehama hususani mitandao ya kijamii  katika kufanya shughuli zenye maendeleo.

Ameyasema hayo  katika kilele cha maadhimisho ya siku ya sheria nchini kwa mwaka huu yenye kauli mbiu isemayo"matumizi ya tehama katika utoaji wa  haki kwa wakati na kwa kuzingatia maadili''

Pia Wela amesema ni wajibu wa kila mmoja kutoa haki katika kuzingatia sheria na kuepuka kuingilia majukumu ya mwingine bali waweze kutekeleza majukumu yao katika nafasi zao kwa ajili ya maendeleo ya wilaya ya Hai na Tanzania kwa ujumla.

Kwa upande wake hakimu mkazi mfawidhi wa Wilaya ya Hai na Siha Anold John Kirekiano amesema katika kutoa haki mahakama inashirikiana na polisi,magereza pamoja na mihimili mingine ikiwa lengo ni kuhakikisha nchi inasonga mbele kwa kufanya kazi kwa kuzingatia maadili.


Pia ameongeza kwa kusema kwamba kama mfumo wa tehama ukitumika kikamilifu utaweza kurahisisha utendaji wa kazi na pia tehama inanafasi zaidi kuhifadhi nyaraka  mbalimbali na ni salama.

No comments:

Watumiaji wa Barabara Watakiwa Kutii Sheria za Usalama

Mkuu wa Kitengo cha Usalama barabarani Mkoa wa Kilimanjaro Mrakibu Msaidizi wa Polisi Sauda Mohamed akizungumza na wananchi kwenye ...