Sunday, 11 February 2018

MGOMBEA UBUNGE AIHIDI NEEMA KWA WAZEE

Na Bahati Chume SIHA

Mgombea ubunge kupitia chama cha wananchi Cuf Tumsifieli Mwanry amesema akichaguliwa atahakikisha Wazee wanapata matibabu bila usumbufu wowote.
  

Akizungumza kwenye mkutano wa kampeni za ubunge kata ya ngarenairobi wilayani Siha, ambapo alisema ataandaa bajeti kwa ajili ya Wazee ili waweze kupata matibabu bila usumbufu wowote.
"wazee wamekuwa wakifika hospitalini wakiwa na vitambulisho lakini wanaambiwa wakanunue dawa kwamba zimekwisha"amesema Tumsifieli.

Ameongeza kwakusema "Mzee hana hela ndiyo maana amepewa kitambulisho lakini anaambiwa akanunue dawa ,nichagueni niweke bajeti kwa ajili ya matibabu ya Wazee" amesema Tumsifieli.

Watumiaji wa Barabara Watakiwa Kutii Sheria za Usalama

Mkuu wa Kitengo cha Usalama barabarani Mkoa wa Kilimanjaro Mrakibu Msaidizi wa Polisi Sauda Mohamed akizungumza na wananchi kwenye ...