Wednesday, 17 January 2018

RAIS DKT. MAGUFULI AKUTANA NA MAWAZIRI WA ELIMU NA TAMISEMI, APIGA MARUFUKU MICHANGO MASHULENI




Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli leo Januari 17, 2018 amepiga marufuku aina yoyote ya michango katika shule za Serikali za msingi na Sekondari nchini.


Raisi Magufuli amepiga marufuku hiyo hiyo leo alipokutana na Waziri Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI) Mhe. Selemani S. Jafo na Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi Profesa Joyce L. Ndalichako Ikulu jijini Dar es salaam na kuwataka mawaziri hao kwenda kusimamia jambo hilo na kuhakikisha hakuna michango yoyote wanafunzi au wazazi wanachangishwa kwenye shule za sekondari.

Nae Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mhe. Selemani Jafo amesema kuwa baadhi ya walimu ambao wamekuwa wakichukua michango ya wazazi na wanafunzi na kuzipeleka kwenye mambo yao binafsi watashughulikiwa.

Waziri Jafo amesisitiza kuwa hatua kali zitaanza kuchukuliwa ndani ya wiki hii na kuwataka wakuu wa mikoa na wakuu wa wilaya kuhakikisha mpaka siku ya Ijumaa wawe wamefikisha taarifa za shule ambazo zilifanya jambo hilo na kukiuka utaratibu wa Serikali. 

Waziri ndalichako ameagiza waalimu na viongozi wa halmashauri kuwarudishu shuleni mara moja wanafunzi wote waliorudishwa nyumbani kwakutotoa michango na pia kurejesha mara moja michango iliyokusanywa kinyume na muongozo wa serikali.

No comments:

Watumiaji wa Barabara Watakiwa Kutii Sheria za Usalama

Mkuu wa Kitengo cha Usalama barabarani Mkoa wa Kilimanjaro Mrakibu Msaidizi wa Polisi Sauda Mohamed akizungumza na wananchi kwenye ...