Monday, 15 January 2018

RAIS DKT.MAGUFULI AWALILIA WATU 11 WALIOKUFA AJALINI MKOANI KAGERA




Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli ametuma salamu za rambirambi kwa mkuu wa Mkoa wa Kagera kufuatia vifo vya watu 11 waliofariki leo kwenye ajali ya gari.



Kwenye taarifa iliyotolewa na Msemaji wa Serikali ambayo imeelezea jinsi Rais alivyoguswa na kusikitishwa na vifo hivyo, na kuwafariji wafiwa katika kipindi hiki kigumu.

"Nimehuzunishwa na kusikitishwa sana na vifo hivi, nawapa pole wafiwa wote na nawaombea marehemu wapumzike mahali pema, na majeruhi wapone haraka ili waweze kuungana na familia zao na kuendelea na shughuli zao za kila siku", imeandika taarifa hiyo.
Isome hapa taarifa yote

No comments:

Watumiaji wa Barabara Watakiwa Kutii Sheria za Usalama

Mkuu wa Kitengo cha Usalama barabarani Mkoa wa Kilimanjaro Mrakibu Msaidizi wa Polisi Sauda Mohamed akizungumza na wananchi kwenye ...