Na Elisha Eliakimu -HAI
Mkuu wa Wilaya ya Hai mshikizi, Onesmo Buswelu amewataka wakuu
katika shule za sekondari na waalimu
wakuu katika shule za msingi kuakikisha wanafunzi wote walioandikishwa na waliochaguliwa kujiunga na kidato cha
kwanza wanaudhuria shuleni pindi shule
zitakapofunguliwa ili waweze kuanza masomo yao.
Ameyasema hayo
leo katika kikao kilichowakutanisha maafisa elimu wa kata
pamoja na waalimu wa shule za msingi na
sokondari wilaya ya Hai, kwa lengo la kujiandaa kufanya maandalizi ya kuuanza
mwaka kitaaluma kwa waalimu kwa kipindi hiki cha kufungua shule.
Aidha Buswelu pia amewataka
makamu wa shule zote za msingi na
sekondari kusaidiana na wakuu wa shule katika usimamizi ili
kuakikisha wanafunzi wanakuwa na nidhamu mashuleni na hata majumbani.
Kwa upande wake afisa elimu
wa shule za sekondari Halmashauri
ya wilaya ya Hai Bw. Julius Kakyama amewataka waalimu wakuu kuhakikisha kuwa siku ya kufungua shule
wanafunzi wote wanaingia darasani kwa ajili ya kuanza masomo yao badala ya kufanya siku
hiyo kuwa siku ya kufanya usafi mashuleni.
‘’kwa sababu tunaanza mwaka ni vizuri zaidi tukajipanga kwa
pamoja tunaanzaje,je wanafunzi wanapokwenda kufungua shule tarehe nane jumatatu
mwezi wa kwanza 2018,wanaanzaje na tukizingatia kwamba siku yakwanza yakufungua
shule ni siku yakuingia darasani na jumla ya siku kwa mwaka za masomo ni 195,na
siku zote lazima wanafunzi waingie darasani,kwa hiyo siku ya kwanza nilazima
watoto waingie darasani”amesema Kakyama.
Ameongeza na kusemaa kuwa shule za sekondari zina uhaba wa
waalimu wa sayansi na hisabati, huku idadi ya waalimu wa sanaa wakiwa ni wengi
hivyo kupelekea kufanya mpango wa kuchukua waalimu wa sanaa katika shule za
sekondari kwaajili ya kufundisha shule za msingi, na kwasasa wanasuburi
mwongozo kutoka taifa ili waseme ni mbinu gani ambazo watatumia.
No comments:
Post a Comment