Friday, 29 December 2017

WANACHAMA CCM KILIMANJARO WATAKIWA KUTOA USHIRIKIANO KWA WANAOJIUNGA NA CHAMA HICHO






Na Kija Elias, siha.

Chama Cha Mapinduzi mkoa wa Kilimanjaro, kimewataka wanachama wa chama hicho kutowatenga wale wote wanaorejea ndani ya CCM, na badaala yake wawape ushirikiano.

Rai hiyo imetolewa jana na Katibu wa CCM mkoa wa Kilimanjaro, Jonathan Mabihya wakati wa hafla ya kuwapokea madiwani watatu waliokuwa kwenye Chama cha Demokrasia na Maendeleo Chadema, pamoja na aliyekuwa Mbunge wa jimbo la Siha Dkt Godwin Molell  ambao wameamua kukihama chama hicho na kurejea ndani ya CCM. 

Mabihya aliwataka wanachama wa CCM kutokujiona wanyonge, pindi pale wanapowaona wanachama kutoka upinzani wakirejea ndani ya CCM, bali wawape ushirikiano kwani moja ya Ilani ya chama hicho ni kuwaunganisha watu pamoja.

Aidha Mabihya amewapongeza madiwani hao kwa uamuzi wao wa kurudi kwenye chama ambacho sera zake zinatekelezeka kuliko huko ambako walikuwa wakishindwa kuwaletea maendeleo wananchi wao kutokana na kutokuwa na serikali.

“Leo tumewapokea ndugu zetu hawa waliorudi ndani ya chama chetu, niwaombe wana CCm kuwapa ushirikiano wa kutosha ndugu zetu hawa na msijione wanyonge wapeni ushirikiano,”alisema.

Katika hatua nyingine chama hicho kimekanusha taarifa ambazo zimekuwa zikienezwa na baadhi ya wanachama wa CHADEMA kuwa kimekuwa kikiwanunua wanachama ili warejee ndani ya CCM.

“Wako watu ambao wamekuwa wakiwaona watu wanaorejea CCM kuwa wamenunuliwa, hizo ni siasa za kupakana matope, dhamira zao ndizo zilizowatuma kurejea ndani ya CCM.

Alifafanua kuwa CCM haijawahi kupanga bei ya kumnunua mtu ili arejee ndani ya CCM, binadamu hana bei    

No comments:

Watumiaji wa Barabara Watakiwa Kutii Sheria za Usalama

Mkuu wa Kitengo cha Usalama barabarani Mkoa wa Kilimanjaro Mrakibu Msaidizi wa Polisi Sauda Mohamed akizungumza na wananchi kwenye ...