Na Kija Elias, Hai.
SERIKALI
imeombwa kuongeza nguvu katika kuimarisha ulinzi kwa watu wenye ulemavu wa
ngozi (Albino), ili nawao waendelee kuyafurahia maisha ya hapa ulimwenguni.
Kauli
hiyo imetolewa na Mwakilishi wa Parokia ya Hai Mjini, Padri Augustino
Ndepanisho, wakati wa Misa ya maadhimisho ya Siku ya watoto Mashahidi
kwenye shule ya Mt. Fransis wa Assis inayowatunza watoto wenye ulemavu wa
ngozi.
Alisema
kuwa serikali bado inawajibu mkubwa wa kuhakikisha inavikomesha vitendo vya
ukatili vinavyoendelea hapa nchini, dhidi ya watu wenye ulemavu wa ngozi
(Albino) vya kuwauwa kwa kuwakata viungo vyao na kwamba wale wote wanaofanya
vitendo hivyo, washughulikiwa kwa mujibu wa sheria.
“Leo
hii katika ulimwengu wetu bado akina Herode wapo na wameongezeka, wanaukatili
mkubwa sana usioelezeka na kwamba wana roho ya ukatili,”alisema.
Naye
Padri Adanthony Marunda wa Jimbo la Moshi, alisema kila Jamii inapaswa kutambua
thamani ya uhai wa kila mtu, kwa kutetea maisha yao ikiwemo kuwapatia
elimu, mavazi pamoja na chakula.
Alisema
wapo baadhi ya watu wamekuwa wakifanya vitendo vya ukatili kwa watu wenye
ulemavu wa ngozi ili waweze kulinda ufalme wa familia zao.
Mkuu
wa mkoa wa Kilimanjaro Anna Mghwira ambaye alifika katika shule hiyo amesema
kuwa serikali ya mkoa imejipanga kuhakikisha kwamba inaweka ulinzi wa kutosha
kwa watoto wenye ulemavu wa ngozi katika shule hiyo.
“Watu
wenye ulemavu wa ngozi bado ni wengi katika mkoa wetu hususan katika wilaya ya
Hai na Siha, hivyo serikali itaweka ulinzi wa kutosha katika shule hii ambayo
inawatunza watoto hawa.
Awali
akipokea misaada mbalimbali kutoka kwa familia ya Patrick Boyi Safi iliyofika
katika shule hiyo na kutoa misaada mbalimbali ya kibinadamu ikiwemo chakula
Mkuu wa shule ya msingi ya Mt. Francis wa Assis Sister
Costantina, ameipongeza familia hiyo kwa kuguswa na changamoto zinazowakabili
watoto hao.
Hata
hivyo Sister Costantina ameiomba serikali kuwapatia askari wenye silaha
watakaoweza kutoa ulinzi kwa watoto hao katika shule hiyo.
Akizungumza
mara baada ya kutoa misaada hiyo Patrick Boyi Safi,amesema ameguswa na
changamoto ya watoto hao wenye ulemavu wa ngozi na kuona kuwasaidia ili na wao
waweze kujiona kwamba jamii haijawatenga.
Mwisho.
No comments:
Post a Comment