Friday, 29 December 2017

MADIWANI WILAYA YA HAI WAAPISHWA






Na, Riziki Lesuya
HAI

Madiwani wateule watatu  katika Halmashauri ya Wilaya ya Hai waliochaguliwa katika uchaguzi mdogo uliofanyika Novemba 26 mwaka huu wameapishwa leo ili kuungana na madiwani wengine katika kuwahudumia wananchi wa wilaya ya Hai.

 
Madiwani walioapishwa ni Mhe. Martin Munisi wa kata ya Machame Magharibi, Mhe. Salehe Msengesi wa kata ya Weruweru na Mhe. Nasibu Mndeme kutoka kata ya Mnadani.

Madiwani hao walikula kiapo hicho mbele ya Hakimu Mkazi wa Mahakama ya Wilaya ya Hai Regina Moshi Katika ukumbi wa Halmashauri likishuhudiwa na wajumbe wa Baraza la madiwani, wataalamu wa halmashauri pamoja na wananchi waliohudhuria kwenye kikao hicho.

Awali akifungua kikao cha Baraza la Madiwani wa Halmashauri hiyo, Mwenyekiti wa Halmashauri Mhe. Helga Mchomvu amewakaribisha madiwani walioapishwa na kuwataka kuongeza nguvu katika jukumu la kuwahudumia wananchi wa Wilaya ya Hai kwa kuzingatia kanuni na taratibu za halmashauri.

Aidha mchomvu amewataka madiwani hao kutambua kuwa halmashauri inaongozwa kwa kanuni na si vinginevyo na kwamba kila mmoja anao wajibu wa kuchangia na kuwa mbunifu katika kuiletea maendeleo Halmashauri.

Amesema kuwa swala la siasa lilimalizika kwenye kipindi cha kampeni na sasa ni wakati wa kutekeleza kilichoahidiwa kwa wananchi.

No comments:

Watumiaji wa Barabara Watakiwa Kutii Sheria za Usalama

Mkuu wa Kitengo cha Usalama barabarani Mkoa wa Kilimanjaro Mrakibu Msaidizi wa Polisi Sauda Mohamed akizungumza na wananchi kwenye ...