Tuesday, 12 December 2017

AOMBA MSAADA WA MALIPO YA MATIBABU BAADA YAKUCHOMWA KISU



Na mwandishi wetu

HAI

Mkazi wa kijiji cha Warisinde kata ya machame Kaskazini Wilayani Hai Mkoani Kilimanjaro Amemu Muru (47)ameomba msaada wa sh,800,000 anazodaiwa katika Hospitali ya Mkwarungo iliyopo machame wilayani humo ili aweze kuruhusiwa kutoka hospitalini hapo.




Akizungumza na Mwandishi  aliko lazwa katika hospitali hiyo,alisema anadaiwa fedha hizo kwa ajili ya matibabu aliyoyapata ili aweze kuruhusiwa kutoka hospitalini hapo.


Muru alisema kuwa amerusiwa kutoka  hospitali wiki mbili zilizopita lakini fedha za kulipa  amekosa hivyo kuomba wananchi mwenye nia ya kumsaidia kuilipa ili aweze kutoka 



Mwanamke huyo alifikishwa Hostalini hapo Novemba 10 mwaka huu baada ya kuchomwa kisu cha mkono wakati akimuokoa binti yake wa kidato cha pili asibakwe na muhuza chipisi



Afisa Tarafa Machame Nsajigwa Nadagile,alisema kwamba mama huyo amekuwa akimpigia simu mara kwa mara kwa ajili ya kuomba msaada wa kulipa fedha za matibu



Kiongozi mmoja  wa Hospitali hiyo ambaye hakutaka jina lake litajwe,alisema wanamdai mama huyo na anachotakiwa ni kulipa iliaweze kuruhusiwa kurudi nyumbani ,lakini jinsi anavozidi kukaa hapo fedha nazo zinaongezeka



Kwa upande wake mwenyekiti wa Kijiji hicho Nasoro Mushi alikiri kuwa mama huyo alichomwa kisu kwenye kiwako cha mkono na kijana anayefahamika Nasoro Ramadhani (24)msambaa mkazi wa kijiji hicho ambaye pia ni muhuza chipsi ,na kwa sasa jambo hilo lipo kwenye vyombo vya seria

No comments:

Watumiaji wa Barabara Watakiwa Kutii Sheria za Usalama

Mkuu wa Kitengo cha Usalama barabarani Mkoa wa Kilimanjaro Mrakibu Msaidizi wa Polisi Sauda Mohamed akizungumza na wananchi kwenye ...