Tuesday, 12 December 2017

WATAKIWA KUBUNI MIRADI YA MAENDELEO



HAI


WAUMINI wa dini ya Kiislamu Nchini wametakiwa kubuni miradi ya maendeleo itakayo wasaidia kukuza kipato cha familia na nchi kwa ujumla




Wito huo umetole  na Shekh Hamis Ame kutoka Dare saalama wakati wa Kongamana la siku tano kiislamu lililofanyia Bomang'ombe wilayani Hai mkoani Kilimanjaro,lengo  kubuni miradiya maendeleo na kuachana na makudi yasiyo eleweka katika dini



Ame alisema ni vyema Waislamu watambue umuhimu wa kushiriki kuanzisha miradi mbali mbali ya maendeleo kama kujenga  Hospitali , shule na viwanda zitakazo wasaidia kukuza kipato  na kuleta maendeleo



''Alisema Waislamu wa frusa nyingi za kuleta maendeleo wamebaki nyuma kutokana na kushindwa kujitoa kuchangia fedha za kutosha kwa ajili ya kuanziasha miradi ya maendeoleo''alisema Ame



Aidha aliwataka waumini hao kusoma na kuielewa dini hiyo iliwasije tumbukia katika makundi mabaya ambayo yanajinasibisha na dini hiyo na kusababisha sintofahamu



''Kuna makundi hapa duniani yanafanya mambo ambayo ni kinyume na mafundisho ya dini yanatakiwa kuondoshwa mara moja au kuyapunguza kabla hayajaleta mazara''alisema Ame



Kwa upande wake Abdlah Juma immamu wa msikiti wa Abuu uliopo Bomang'ombe aliwataka waislamu kuzingatia elimu ili kwenda sambamba na Tanzania ya viwanda.



Waumini tunatakiwa kusoma na kuwa wabunifu wa mawazo mapya yatakayo waletea maendeleo bora na kukuza uchumi wetu na Nchi kwa ujumla kuliko kukaa na kupika majungu yasiyo na tija.

No comments:

Watumiaji wa Barabara Watakiwa Kutii Sheria za Usalama

Mkuu wa Kitengo cha Usalama barabarani Mkoa wa Kilimanjaro Mrakibu Msaidizi wa Polisi Sauda Mohamed akizungumza na wananchi kwenye ...