Mkuu wa Wilaya Ya Hai Mh. Onesmo Buswelu katikati akisikilza maelezo kutoka kwa kamati ya shule ya sekondary Longoi iliyopo kata ya weru weru wilayani Hai mara baada yakufika shuleni hapo. |
Kamati ya shule ya Sekondary Longoi wakimsikiliza kwa umakini mkuu wawilaya ya Hai Onesmo Buswelu baada yakutembelea shuleni hapo. |
Na Davis Minjer_ Hai
WANANCHI Wilayani Hai Mkoani Kilimanjaro wametakiwa
kushiriki na kuhimiza shughuli za maendeleo katika maeneo yao,hasa katika sekta
ya elimu ili kuandaa kizazi cha wasomi wa kusaidia Taifa na siyo kufuata kila
linalo semwa na wanasiasa wanaopinga maendeleo.
Rai
hiyo imetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Hai Onesmo Buswelu wakati akizungumza na
kamati ya shule ya sekondari Longoi iliyopo kata ya weruweru kwaajili ya
kufufua jitihada za kuchangia ujenzi wa vyumba vya madarasa ili kupunguza adha
wanazo pata wanafunzi na waalimu wakati wa kutimiza majukumu yao.
Kwa
upande wake Kaimu Mwalimu Mkuu wa shule hiyo Jasper Mbwambo amebainisha
changamoto zilizopo katika shule hiyo ikiwemo upungufu wa madarasa tisa hali
inayo pelekea wanafunzi 80 kutumia chumba kimoja hali inayo leta usumbufu.
Kwa
upande wake Mjumbe wa kamati ya Shule hiyo Suleman mvungi amebainisha kuwa
kusuasua kwa shughuli ya maendeleo katika kata hiyo ni kutokana na wananchi
kuingiza siasa kwa kila maamuzi ya kufikia maendeleo jambo linalo kwamisha hata
vikao vyao ndani ya kijiji.
Shule
ya Sekondari longoi ina wanafunzi 852 ikiwemo wanafunzi 245 kidato cha
kwanza,377 kidato cha pili,126 kidato cha tatu na 104 kidato cha nne jambo
linalo pelekea kuwa na ukosefu wa vyumba vya madarasa tisa kutokana na sasa
kuwa na vyumba vya madarasa 12 tu.
No comments:
Post a Comment