Wednesday, 11 April 2018

TASAF yazidi kuwanufaisha kaya masikini Hai


Na Omary Mlekwa

HAI

WANUFAIKA wa mpango wa kunusuru kaya maskini unaondeshwa na mfuko wa jamii (TASAF) wameshauriwa  kutumia fedha wanazopata kuanzisha shughuli za ujasiriamali ili kuondokana na hali tegemezi .


Ushauri huo umetolewa na Bi  Sophia Gao mkazi mtaa wa Kia wilayani Hai mkoani Kilimanajro wakati akielezea mafanikio aliyoyapata kutokana na fedha anazozipata kupitia TASAF, jinsi zilivyoweza kubadilisha maisha yake.
Bi Gao amesema  endapo wanufaika na mpango huo wataweza kutumia fedha hizo kwa malengo zitawasadia kuboresha hali ya maisha yao  kuondokana na hali tegemezi pindi mradi huo unapofikia mwisho.

Amesema kuwa anaishukuru  serikali  kwa kumwezesha  kubadilisha maisha yake ambapo awali alikuwa akiishi maisha ya  tabu kutokana na kutokuwa na uwezo wa kuendesha maisha  na familia lakini kwa sasa  maisha yake yamebadilika  kabisa.

Aidha Bi Gao amefafanua kuwa fedha alizopata tangu kuanzishwa kwa mpango ameweza kuanzisha mgawaha pamoja na kibanda cha kuuzia matunda na mboga mboga  jambo ambalo limemsaidia kuendesha familia yake pamoja na kuweza kununua eneo kwa ajili ya kujenga nyumba ya kuishi.

Naye Bi Grace Macha ambaye  pia ni mnufaika amesema fedha alizopata kwa awamu 17 kutoka TASAF ameweza kuanzisha ufugaji wa kuku pamoja na mbuzi hali iliyosaidia kuboresha maisha yake ambapo hapo awali alikuwa akiishi kwa mlo mmoja lakini kwa sasa ana uwezo wa kula mara tatu kwa siku.

Kwa upande wake, mratibu wa TASAF wilaya ya Hai  , Bwana Erick Marishamu amesema tangu zoezi hilo lianzishwe  jumla  ya shilingi bilioni 2.5 zimetumika kunufaisha kaya 3905 katika vijiji 43 vilivyoko kwenye mpango huo.

No comments:

Watumiaji wa Barabara Watakiwa Kutii Sheria za Usalama

Mkuu wa Kitengo cha Usalama barabarani Mkoa wa Kilimanjaro Mrakibu Msaidizi wa Polisi Sauda Mohamed akizungumza na wananchi kwenye ...