Na Davis Minja
HAI
Wazazi na Walezi Wilayani Hai Mkoani Kilimanjaro wametakiwa kuacha tabia ya kuwatelekeza watoto katika shule wanazo soma pasipo kuwa nao karibu, hali inayosababisha watoto kukosa upendo na malezi kutoka kwa wazazi.
Wazazi na Walezi Wilayani Hai Mkoani Kilimanjaro wametakiwa kuacha tabia ya kuwatelekeza watoto katika shule wanazo soma pasipo kuwa nao karibu, hali inayosababisha watoto kukosa upendo na malezi kutoka kwa wazazi.
Rai hiyo imetolewa na Mkuu wa Wilaya ya Hai mshikizi Onesmo Buswelu wakati akikabidhi mifuko 75 ya saruji iliyo kuwa imeahidiwa na Mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro Anna Mghwira katika ujezi wa Bweni la Wanafunzi wa Shule ya St.Fransis Wa Sisi.
Kwaupande wake Mwalimu mkuu wa Shule hiyo Sister Costantine Mosha amekiri kuwepo kwa baadhi ya wazazi na walezi wanao kimbia majukumu ya kuwalea watoto wao na badala yake wanatumia fursa ya elimu kuwatelekezea wanafunzi shuleni huku wengine wakibadili namba za simu kuepuka kufuatiliwa.
WAKATI HUO HUO
Jeshi la polisi wilayani Hai mkoani Kilimanjaro limeweka mikakati kuhakikisha linadhibiti vitendo vya utoaji mimba kwa wanafunzi kwani ni hatari kwa maisha yao na jamii kwa ujumla.
Jeshi la polisi wilayani Hai mkoani Kilimanjaro limeweka mikakati kuhakikisha linadhibiti vitendo vya utoaji mimba kwa wanafunzi kwani ni hatari kwa maisha yao na jamii kwa ujumla.
Akizungumza na Redio Boma FM Mwenyekiti wa dawati la jinsia wilayani Hai Happy Eliufoo amesema kwa sasa wameanza kutoa elimu katika shule mbalimbali wilaya ya Hai kwa lengo la kudhibiti vitendo hivyo kwani ni kinyume cha sheria.
Kwa upande wao walimu katika shule ya Sekondari Hai wamesema wameanza kudhibiti suala hilo kwa kuchukua hatua ya kuwapima ujauzito wanafunzi ambapo suala hilo hufanyika kwa kila mwaka kwa awamu mbili.
Nao baadhi ya wanafunzi wa shule hiyo wamesema kuwa pindi wanapopata mimba hulazimika kutoa ili waweze kuendelea na elimu kutokana na agizo la Rais Dr.Magufuli kuwa mwanafunzi wa kike atakapopata ujauzito atalazimika kukatisha masomo yake haraka iwezekanavyo licha ya kufahamu kwamba kufanya hivyo ni hatari kwa maisha yao.
Aidha baadhi ya wazazi wamezungumzia suala hili na kusema kuwa ni hatari na hakuna mzazi anayefurahi mwanaye kufanya vitendo hivyo ambavyo pia ni kinyume na sheria za dini
No comments:
Post a Comment