Saturday, 24 February 2018

Shule Yafungwa Kwa Muda Usiojulikana

Na Omary Mlekwa
Hai

Serikali Mkoani Kilimanjaro imeifunga shule ya msingi Kibohehe iliyopo wilaya ya Hai kwa mda usijulikana ili kupisha ukarabati wa shule hiyo  kutokana na baadhi ya miundombinu yake  kuharibiwa vibaya na mvua na upepo .


Mkuu wa Mkoa huo,Anna Mghwira alitoa agizo hilo baada ya kutembelea shule hiyo kujionea uharibifu uliotekea  hali ambayo ilisababisha mwanafunzi mmoja wa dasasa  la  sita kupoteza maisha huku wengine watatu wakijeruhiwa vibaya.

Alisema uamuzi huo unatokana na kubaini kuwa ujenzi wa vyumba vya madarasa katika shule hiyo umejengwa chini ya kiwango jambo ambalo  lisipoangaliwa kwa umakini linaweza kusababisha madhara wengine kwa wanafunzi  na watumishi wa shule hiyo.

"Tunafunga shule hii ili kupisha ukaratabi wa majengo  na wanafunzi  kuanzia darasa la  awali hadi darasa la  saba watatawanywa katika shule nyingine za jirani mpaka pale ukarabati utakapokamilika" alisema Mghwira
"Wataalamu wa Halmashauri watafanya  tathmini ya ukarabati na kutueleza mda halisi lakini pia ukarabati huo ,utakuwa na malengo wawili ya mda mrefu na mfupi ili wanafunzi warejee na kuendelea na masomo yao." alisisitiza

"Licha ya kufunga shule pia ujenzi wa shule hiyo ,ulijengwa chini ya kiwango na bila kufuata utaratibu za ujenzi  agizo kukamatwa kwa msimamizi wa ujenzi pamoja na aliyekuwa mwalimu mkuu  wa shule kipindi  ujenzi ulipofanyika" aliongeza 

"Chanzo kikuu cha kuezuliwa kwa bati  la  chumba cha darasa la  tatu ni kutokana na kujengwa chini ya kiwango na kukosekana kwa umakini pindi ujenzi ulipofanyika"

"Majengo haya yamejengwa chini ya kiwango na hayakufuata kanuni za ujenzi tena hayajafungwa lenta hali ambayo imesababisha kubomoka kwa utahisi " alisema Mghwira 

Kwa upande wake mhandisi wa Halmashauri hiyo, Loshiwa Moleli alisema kuwa shule hiyo ilijengwa zamani na tayari walishashauri kuwa majengo  hayo yavunjwe ili kuepuka madhara
"Mheshimiwa tayari tulishakagua majengo  yamejengwa chini ya kiwango na tulishauri yajengwe mapya " alisema Moleli

Nae Mwalimu Mkuu wa shule hiyo,Aileni Lema alisema changamoto kubwa ni upungufu wa madarasa ambapo mpaka sasa wanavyumba sita vya madarasa ambavyo  vinatumiwa na wanafunzi  wa darasa la  awali mpaka darasa la  saba.

"Shule yetu ina  wanafunzi  162 na haina vyumba vya madarasa ya awali na darasa la  kwanza jambo linapelekea tutumie hata haya madarasa ambayo yamejengwa chini ya kiwango" alisema

No comments:

Watumiaji wa Barabara Watakiwa Kutii Sheria za Usalama

Mkuu wa Kitengo cha Usalama barabarani Mkoa wa Kilimanjaro Mrakibu Msaidizi wa Polisi Sauda Mohamed akizungumza na wananchi kwenye ...