Monday, 26 February 2018

HALI NGUMU YA BIASHARA YAZIDI KUTIKISA WAFANYA BIASHARA WILAYANI HAI



NA mwandishi; ZAINA ANDREA




HAI

Wafanyabiashara wadogo wadogo katika eneo la stendi ya Sanya juu wilayani hai wanapambana na hali ngumu ya biashara kutokana na kupanda kwa bei za bidhaa mbalimbali masokoni.

Akizungumza na radio boma fm mjasiriamali na mfanya biashara Jesca James, amesema kuwa kwa sasa wanafanya biashara kwa lengo la kulinda mtaji kutokana na hali ngumu ya biashara na wala sikwaajili ya kupata faida.

Amesema kupanda kwa bei ya Nyanya, vitunguu,matunda pamoja na usafirishaji wa bidhaa hizo pia ni changamoto kwao kwani wanafanyakazi bila ya kipato kinachowaridhisha katika kazi zao.

Aidha wamesema pamoja na hayo wanaendelea vizuri katika kutunza mazingira ya maeneo hayo kwa kutii sheria na taratibu zilizowekwa na serikali ya mamlaka ya mji mdogo wa Bomang’ombe.

Pia  Wameiomba serikali iwasaidie kwa kuwawezesha katika biashara zao ili kuendelea kijikimu kimaisha kupitia biashara zao za kila siku.

No comments:

Watumiaji wa Barabara Watakiwa Kutii Sheria za Usalama

Mkuu wa Kitengo cha Usalama barabarani Mkoa wa Kilimanjaro Mrakibu Msaidizi wa Polisi Sauda Mohamed akizungumza na wananchi kwenye ...