Wednesday, 3 January 2018

Jaffo aipongeza Hai



 
Waziri  Suleiman Jaffo akisalimiana na wakuu wa idara mbali mbali katika Halmashauri ya Wilaya  ya Hai

Na Adrian Lyapembile_HAI


WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (TAMISEMI)Mhe. Selemani Jaffo ameipongeza halmashauri ya wilaya ya hai kwa kuendelea kuboresha miundombinu katika hospitali ya wilaya hiyo itakayofanikisha azma ya serikali ya kutoa huduma bora za afya kwa wananchi wake.

Mhe. Jaffo ameyasema hayo kwenye ziara yake ya kikazi katika wilaya ya Hai ambapo ametembelea hospitali ya wilaya hiyo kukagua utekelezaji wa miradi ya maendeleo ikiwemo ujenzi wa wodi ya magonjwa mchanganyiko, ununuzi wa jenereta la kisasa la kufua umeme pamoja na ujenzi wa duka la dawa.

Amesema hatua iliyofikiwa ni nzuri kwenye ujenzi wa jengo la wagonjwa mchanganyiko na duka la dawa huku akiongeza kuwa uwepo wa duka la dawa la kuaminika katika wilaya ni jambo jema ambalo litasaidia wananchi wa wilaya ya Hai na maeneo jirani kupata dawa kwa uhakika.

Mapema akitoa maelezo ya ujenzi huo Mkurugenzi Mtendaji wa halmashauri ya wilaya ya Hai Yohana Sintoo amemwambia waziri Jaffo kuwa ujenzi wa duka la dawa umekamilika na kwamba kinachofanyika kwa sasa ni kuweka samani pamoja na kufunga vifaa vinavyohitajika.

Naye Kaimu Mganga Mkuu wa Wilaya Dk. Irene Haule amesema pamoja na kuwa jengo hilo limejengwa maalumu kwa ajili ya wanachama wa bima za afya lakini litatumika kama kitega uchumu kwa hospitali hiyo ambapo litatoa huduma kwa wagonjwa wengine wasio wanachama wa bima ambao watanunua dawa lengo kuu likiwa ni kuondoa tatizo la kukosekana dawa kwenye hospitali ya wilaya na maeneo ya jirani.

No comments:

Watumiaji wa Barabara Watakiwa Kutii Sheria za Usalama

Mkuu wa Kitengo cha Usalama barabarani Mkoa wa Kilimanjaro Mrakibu Msaidizi wa Polisi Sauda Mohamed akizungumza na wananchi kwenye ...