Wednesday, 27 December 2017

TRA KILIMANJARO YATEKELEZA AGIZO LA RAISI




Na mwandishi wetu. Hai. 

Mamlaka ya mapato TRA, mkoani Kilimanjaro, imetekeleza maagizo yaliyotolew hivi karibuni na  Rais Dkt John Magufuli ambayo iliwataka Mamlaka hiyo, kuhakikisha wanafunga mashine ambayo itadhibiti mapato yanayotokana na mizigo inayoingizwa ndani na nje ya nchi kupitia uwanja wa ndege wa Kimataifa KIA. 


Akiongea wakati wa ufungaji wa mashine hiyo mpya Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Anna Mghwira, alisema kuwa uwepo wa mashine hiyo pia utasaidia uwezekano wa kupotea kwa mapato ya serikali katika uwanja huo.

 “Mashine hii itasaidia kudhibiti aina zote za upotevu wa mapato ya serikali, kwani inaweza kukagua mizigo inayoingizwa nchini na ile inayotoka n kufanyiwa makadirio mbalimbali kwa ufanisi zaidi”, alisema.

Aidha alisema mashine hiyo italeta uwazi na utoaji wa huduma ulio bora na wenye kuzingatia haki.

Aidha aliipongeza TRA kwa jitihada zake za makusudi zinazolenga kuziunga juhudi za Rais Dkt Magufuli katika kulinda mapato ya Taifa. 

Kwa upande wake Meneja wa TRA Mkoa wa Kilimanjaro, Msafiri Mbibo, alisema kuwa mashine hiyo mpya itasaidia kuboresha usalama wa raia kwa kuhakikisha mizigo yote inakaguliwa ili kujua inayo stahiki zote.

“Pia zitasaidia kurahisisha shughuli za wasafiri wanaoingia na kutoka nje ya nchi kwa kutumia uwanja wa ndege na mipaka yetu”, alisema.

Alisema pia zitasaidia kutoa huduma za haraka kwa wasafiri na mali zao, waagizaji wa bidhaa, mizigo na mali mbalimbali na wale wanaopeleka nje ya nchi.

 “Mashine hii itasaidia kugundua endapo abiria atakuwa amebeba dawa za kulevya, madini kinyume cha sheria, nyara za serikali kama vile pembe za ndovu, vilivyofichwa ndani ya begi”, alisema.


Kwa upande wake Kimu Mkurugenzi wa uendeshaji wa kiwanja cha ndege KIA Mhandisi, Martin Kinyamagoha, alisema kuwa mshine hiyo itasaidia sana kupunguza msongamano wa abiria katika uwanja huo kutokana iliyokuweko moja na ilikuwa ni ndogo.

Nae Mkuu wa TRA uwanja wa KIA Elias Njata, alisema kuwa mashine hiyo itasaidia usafirishaji na utorosha madini na nyara zingine za serikali ikiwemo pembe za ndovu.

No comments:

Watumiaji wa Barabara Watakiwa Kutii Sheria za Usalama

Mkuu wa Kitengo cha Usalama barabarani Mkoa wa Kilimanjaro Mrakibu Msaidizi wa Polisi Sauda Mohamed akizungumza na wananchi kwenye ...