Wednesday, 27 December 2017

ASHIKILIWA KWA KUSAFIRISHA MIHADARATI







Na mwandishi wetu MOSHI

JESHI la polisi mkoani Kilimanjaro, linamshikilia mfanyakazi mmoja wa shirika la Umma la Mifuko wa Hifadhi ya Jamii (PPF, kwa tuhuma za kujihusiha na usafirishaji wa dawa za kulevya.

Akidhibitisha kukamatwa kwake, kamanda wa polisi mkoani Kilimanjaro Hamis Issa, alimtaja mtu huyo kuwa ni Anitha Oswald (32) ambaye ni mfanyakazi wa Shirika mifuko wa hifadhi wa PPF, mkoani Kilimanjaro.

“Askari wakiwa doria walimkamata Anitha Oswald, ambaye ni mkazi wa Karanga, Manispaa ya Moshi, akiwa anasafirisha dawa za kulevya aina ya mirungi kilo 216 na gramu 370”, alisema kamanda Issa.

Alisema kuwa mtuhumiwa huyo alikamatwa akisafirisha mirungi hiyo kwa kutumia gari lake analolimiliki mwenyewe lenye namba za usajili T 674 DLB, aina ya Toyota Sienta rangi ya silva.

Kamanda Issa alisema Anitha Oswald alikamatwa eneo la Majengo kwa Mtei Disemba 19, mwaka huu, akiwa anatokea Njia Panda ya Himo kuchukua mzigo huo.

Aidha kamanda Issa alisema kwamba usafirishaji wa dawa za kulevya bado ni changamoto kubwa ambapo alielezea kusikitishwa na tabia ya baadhi ya watumishi wa Umma kujihusisha na usafirishaji huo.

“Jeshi la polisi mkoani hapa liko makini, operesheni inaendelea na hatutamvumilia mtu yeyote ambaye atabainika kujihusisha na biashara hii”, alisema.

Hata hivyo kamanda aliongeza kusema kwamba jeshi hilo la polisi mkoni humo, bado linaendelea kumtafuta dereva wa gari hilo, ambaye alikimbia baada ya kulitelekeza gari alilokuwa akiliendesha baada ya kugonga mti katika jitihada za kuwakimbia polisi.

No comments:

Watumiaji wa Barabara Watakiwa Kutii Sheria za Usalama

Mkuu wa Kitengo cha Usalama barabarani Mkoa wa Kilimanjaro Mrakibu Msaidizi wa Polisi Sauda Mohamed akizungumza na wananchi kwenye ...