NGOMBE
ELFU 68 KUPIGWA CHAPA WILAYANI HAI.
Zoezi la upigaji chapa ng'ombe Wilayani Hai likiwa linaendelea katika kijiji cha Sanya Station Mkoani Kilimanjaro (pcha na Omary Mlekwa) |
NA
OMARY MLEKWA NA QUEEN NDOSY, -Hai
ZAIDI
ngombe elfu 68 zinatarajiwa kupigwa chapa katika zoezi lililoanza kwenye
Halmashauri ya wilaya ya Hai mkoani Kilimanjaro ili kutekeleza Agizo la wizara ya Mifugo na
Uvuvi ambapo linatarajiwa kukamilika Desemba 30 mwaka huu.
Hayo yamebaishwa na mkurugenzi mtendaji wa Halmashauri hiyo, Ndg Yohana Sinto wakati akizungumza na wafugaji wa kijiji cha Sanya Station Kata ya Kia alipotembelea kujionea zoezi hil.
Alisema
kuwa kuna kila sababu kwa wakazi wa wilaya ya Hai haswa wafugaji kujitokeza kwa
wingi kushiriki zoezi hilo ili kuwezesha wanyama wao kupigwa chapa kutokana na
umuhimu wa zoezi hil.
<
Zoezi hili ni muhimu ni sana kwa wakazi
wa wilaya yetu ya Hai kwani tunatambua jinsi mifugo kutoka nje imekuwa
ikitusumbua kutokana na kutokuwa na alama inayoweza kutambulisha mifugo yetu ,
naomba tutumie fursa hii vizuri ;alisema Sintoo.
Alisema
kuwa kukamilika kwa zoezi hilo itasaidia kutambua mifugo iliyopo kwani wilaya
imekuwa na migogoro ya mara kwa mara kati ya wakulima na wafugaji kutokana na
wimbi kubwa la mifugo kutoka wilaya za jirani na hata wafugaji kutoka nje kuvamia mashamba ya wakulima kwa ajili ya
malisho.
Hata
hivyo aliwataka wafugaji wote kutoa mifugo yao na kupigwa kwa muda huu na mara
baada ya kukamilika kwa zoezi hilo wataanza kuwachukulia hatua wale ambao
watashindwa kutekeleza agizo hil.
Kwa upande
wake afisa mifugo wa wilaya ya Hai, Elia Machange tangu kuanza kwa zoezi hilo
wamekuwa wakikabiliwa na changamoto ya kuni za kuchomea chombo kimachumika kwa
ajili ya kupigia chapa ngombe.
Aidhani
amesema kutokana na matumizi makubwa ya kuni wamejipanga kuhakikisha kuwa zoezi
hilo halikwami kwa kushirikiana na viongozi wa vijiji kutoa ushirikiano wao wa
ili kukabiliana tatizo hilo na huduma
iendeele kutolewa kwa muda wote.
Nae kiongozi wa kimila wa kabila wa wafugaji
katika eneo hilo Thomas Sinyoki alisema
zoezi litasaidia kujua ngombe watakaovamia maeneo yao kwani mifugo yao itakuwa
na chapa ya wilaya ya Hai
Sinyoki
alisema pia kupigwa chapa kwa ngombe hao itasaidia kuondoa mwingiliano wa
mifugo kwa wilaya nyingine jambo ambalo litawasaidia katika kuhifadhi sehemu za
malisho.
No comments:
Post a Comment